Search This Blog

Friday, August 27, 2021

Ruto abadilishiwa maafisa usalama asema ni kinyume cha utaratibu



Baada ya Maafisa wa Usalama wa GSU (General Service Unit) kuondolewa katika Makazi ya Naibu Rais wa Kenya, William Ruto, Ofisi ya Kiongozi huyo imesema kitendo hicho ni kinyume cha utaratibu


Imedaiwa kuwa ni mwendelezo wa jitihada za kudhoofisha Usalama Binafsi wa Naibu Rais kwasababu za kisiasa. Pia, ni mkakati unaotajwa kumuweka hatarini


Hata hivyo Jeshi la Polisi limesema Maafisa hao wamebadilishiwa majukumu na wengine (Government Building Unit) watalinda makazi ya Naibu Rais, utaratibu ambao ni wa kawaida kuongeza ufanisi



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...