Search This Blog

Tuesday, August 24, 2021

Rais wa Tunisia: ''Hakuna njia ya kurudi nyuma''


Rais wa Tunisia Kays Said, akielezea uaminifu wake kwa maamuzi ya hivi karibuni yaliyochukuliwa nchini, alisema, "Hakuna njia ya kurudi nyuma."

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, Waziri wa Mambo ya Afrika wa Saudi Arabia, Ahmed Kattan, ambaye alitembelea nchi hiyo, alipokea wajumbe wake katika Ikulu ya Carthage.

Wakati wa mkutano huo, Rais wa Tunisia Kays Said aliishukuru Saudi Arabia kwa msaada wake katika kipindi hiki kigumu hususan nyanja za kisiasa, uchumi na afya nchini mwake.

Akitetea maamuzi yake ya hivi karibuni, Said alisema, "Hakuna njia ya kurudi nyuma." Alidai kwamba maazimio hayo yalilenga kuilinda nchi kutokana na anguko lisilokuwa la kawaida na kumaliza mateso na umasikini wa watu.

Nchini Tunisia, ambapo vuguvugu la Kiarabu ilianza, mzozo unaoendelea wa kijamii, kiuchumi na kisiasa na hali katika mfumo wa afya kwa sababu ya janga la corona (Kovid-19) ilisababisha Watunisia kuingia mitaani kwa maandamano mnamo Julai 25.

Wakati wa maandamano, kulikuwa na athari kali kwa siasa zilizowekwa nchini. Katika mikoa mingine, makao makuu ya Harakati ya Ennahda, chama kikubwa zaidi katika Bunge hilo, yalishambuliwa.

Rais Kays Said alitangaza kwamba alikuwa ametekeleza Kifungu cha 80 cha Katiba, ambacho kilimpa nguvu za mamlaka.

Said alitangaza kuwa amesimamisha kazi za Bunge kwa siku 30, na kwamba kinga ya wabunge wote imeondolewa, na akamfukuza kazi waziri mkuu na atamteua waziri mkuu mpya, na pia akajiteua mwenyewe kama mwendesha mashtaka mkuu wa kesi za ufisadi.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...