Siti Sarah Raisuddin aliyekuwa mja mzito alikuwa amekumbwa na uhaba waoksijeni na aliwekwa kwenye coma ili aweze kujifungua kupitia upasuaji.
Mtoto aliokolewa, ingawa hakuweza kumshika mwanae.
Mumewe alisema alimpigia simu ya mwisho ya video kabla ya kifo chake, ambapo machozi yalikuwa yakimtiririka mashavuni mwake.
"(Ni) kana kwamba alielewa tunachomwambia," mchekeshaji Shuib Sepahtu aliwaambia waandishi wa habari. "Ni kwamba tu itakuwa vigumu sana kwangu kutoa habari kwa watoto wangu watatu juu ya kifo cha mama yao."
Mbali na mtoto huyo mchanga, wenzi hao wana watoto wakubwa watatu wenye umri wa miaka sita hadi 10.
Ripoti zinasema kwamba familia nzima ilikuwa imepatikana na Covid-19 mnamo 25 Julai, baada ya kuambukizwa kutoka kwa msaidizi wao wa nyumbani.
Siku chache baadaye, Siti Sarah alikuwa ameweka video kwenye Instagram ya watoto wake wakilia baada ya kupata vipimo vya Covid.

No comments:
Post a Comment