Search This Blog

Saturday, August 28, 2021

Mchungaji aliyegoma kupeleka Watoto shule akidai Mungu anazuia, ahukumiwa

Mahakama ya Wilaya Bukoba imemtia hatiani Mchungaji Merchades Buberwa mkazi wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kwa makosa matatu kati ya nane yaliyokuwa yakiwakabili yeye pamoja na mke wake yakiwemo makosa ya Sheria ya mtoto na kushindwa kutimiza wajibu wao kama wazazi kwa kutowapeleka watoto shule.

Mchungaji huyo amehukumiwa kifungo cha miezi sita faini ya shilingi milioni moja kwa kila kosa huku mke wake akipewa kifungo cha nje na masharti ya kutotenda kosa lolote ndani ya kipindi cha miezi sita.

Akiongea nje ya Mahakama Wakili wa Serikali ameeleza kwa undani juu ya kesi hiyo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...