Search This Blog

Monday, August 30, 2021

Kiongozi wa Palestina Abbas akutana na waziri Gantz wa Israel


Kiongozi wa mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas amekutana na mwakilishi wa ngazi ya juu wa serikali ya Israel, mkutano huo ukiwa wa kwanza kufanyika kwa muda mrefu baina ya wawakilishi wa nchi hizo mbili.

Ofisi ya Waziri wa Ulinzi wa Israel Benny Gantz imethibitisha katika taarifa kuwa, waziri huyo wa ulinzi alikutana na Mahmoud Abbas mjini Ramallah Jumapili jioni, na walijadiliana juu ya sera za kiusalama, kiraia na masuala ya uchumi miongoni mwa masuala mengine.

Gantz alimwambia Abbas kuwa Israel inataka kuchukua hatuaza kuimarisha uchumi wa Palestina. Viongozi hao wawili walikubaliana kujadiliana zaidi juu ya masuala hayo.

Mkuu wa kitengo cha uratibu wa shughuli za serikali wa Israel Ghasan Alyan na mkuu wa idara ya Ujasusi wa Palestina Majid Faraj pia walishiriki kwenye mkutano huo.

Mkutano huo umefanyika muda mfupi tu baada ya Waziri Mkuu wa Israel Naftali Bennett kurejea kutoka nchini Marekani ambako alikutana na Rais Joe Biden na maafisa wakuu wa serikali ya Marekani.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...