Search This Blog

Friday, August 20, 2021

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ataka mapigano kusitishwa Ethiopia



Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka tena kusitishwa mapigano mara moja katika eneo la Ethiopia la Tigray, ambapo vikosi vya serikali na wapiganaji waasi wamekuwa katikamizozo tangu Novemba mwaka jana

António Guterres alielezea hali ya kibinadamu huko Tigray kama "mbaya" na akasema mashirika ya misaada yanahitaji kufika katika eneo hilo bila vikwazo.

"Mazungumzo kama haya yanaweza kuchangia kushughulikia sababu za msingi za mzozo na kuhakikisha sauti za Waethiopia zinaleta njia ya amani," alisema.

Mamilioni ya watu wamehama makazi yao na mamia ya maelfu wanaishi katika hali ya njaa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...