Search This Blog

Monday, August 2, 2021

Iran yasema haikuishambulia meli karibu na Oman


Iran imekanusha madai kwamba imehusika katika shambulizi linaloshukiwa kufanywa kutumia ndege inayoendeshwa bila rubani dhidi ya meli ya kibiashara yenye mafungamano na Israel katika ghuba ya Oman lililosababisha vifo vya wafanyakazi wawili. 
 
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran, Saeed Khatibzadeh amesema Iran imelaani madai hayo yasiyo na msingi kutoka kwa Israel, akisema utawala wa taifa hilo umesababisha tu machafuko na hali ya wasiwasi. 
 
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Israel Yair Lapid awali aliinyoshea kidole cha lawama Iran kwa shambulizi hilo la mwishoni mwa wiki iliyopita akiandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kwamba Iran sio tu tatizo la Israel, bali pia ni msafirishaji wa ugaidi, uharibifu na uyumbishaji unaowaathiri wote. 
 
Marekani na Uingereza zimeungana na Israel kuilaumu Iran kwa hujuma hiyo, huku Marekani ikiapa kuchukua hatua stahiki.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...