Mkuu wa wilaya ya Kibaha Sarah Msafiri, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Kibaha Butamo Ndalawa, kumsimamisha kazi afisa mazingira wa mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi baada ya kushindwa kusimamia usafi katika eneo hilo.
Mbali na agizo hilo, DC Sarah pia akaweka zuio kwa wafanyabiashara wanaoendesha biashara zao pembezoni mwa barabara kusitisha shughuli zao mpaka pale watakapofanya usafi katika mifereji inayopitisha maji.

No comments:
Post a Comment