Search This Blog

Tuesday, August 3, 2021

China yasitisha shughuli za usafiri kwa baadhi ya maeneo ya Beijing


Usafiri kwenda Beijing, mji mkuu wa China, ulisitishwa ndani ya wigo wa hatua dhidi ya corona (Kovid-19).

Kulingana na taarifa ya South China Morning Post, ili kuzuia kuenea kwa virusi aina ya Delta vya Kovid-19 huko Beijing, baadhi ya ndege za kwenda jijini pamoja na huduma za treni na mabasi zilisimamishwa.

Zaidi ya watu 350 wameambukizwa virusi katika miji 27 baada ya aina mpya ya Kovid-19 inayoambukizwa kwa kasi zaidi kuripotiwa kwa mara ya kwanza katika mji wa Nanjing, mkoa wa Jiangsu mashariki mwa China.

Akizungumza kwenye mkutano wa Chama cha Kikomunisti katika mji mkuu, Katibu wa Chama Jai Qi alisema kuwa mji mkuu unapaswa kulindwa "kwa gharama yoyote", na hatua za haraka zaidi na kali kuamuliwa.

Wakati kesi 4 zimeripotiwa kutoka Beijing hadi kufikia sasa, viongozi wa jiji wamekubali kuongeza hatua za vizuizi za kuingia kwa watu wanaokwenda mji mkuu kutoka maeneo hatarishi, kama tahadhari dhidi ya kesi mpya ambazo zinaweza kutoka maeneo ya karibu.

Kama sehemu ya hatua hizo, kila mtu katika miji ambayo virusi aina ya Delta vya Kovid-19 viligunduliwa alikuwa amepigwa marufuku kuingia mji mkuu wa Beijing, na huduma za usafiri wa ndege, treni na mabasi ya mijini kutoka katika maeneo haya zilisimamishwa.

Ilionekana kwenye maeneo ya kuhifadhi nafasi kwamba tikiti za treni hazikuwepo kwa mikoa ya Nanjing na Zhangjiajie, ambapo virusi vilikuwa vikienea.

Wafanyikazi wa taasisi za serikali na biashara zinazomilikiwa na serikali walipigwa marufuku kusafiri kwenda miji iliyo na virusi, na taasisi zilikatazwa kusafiri kwenda katika mikoa hii.

Wakazi wa Beijing katika moja ya miji hii hawataweza kurudi jijini bila karantini ya siku 14 na matokeo yanayoonyesha hawana maambukizi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...