Search This Blog

Thursday, August 5, 2021

Bolsonaro kuchunguzwa kwa madai ya wizi wa kura


Mahakama ya juu kabisa ya Brazil imeamuru rais wa nchi hiyo Jair Bolsonaro achunguzwe kwa madai ambayo hayajathibitishwa kwamba mfumo wa kupigia kura wa Brazil unagubikwa na udanganyifu. 
 
Hukumu iliyotolewa na jaji Alexandre de Moraes imetolewa baada ya Bolsonaro kuongeza ukosoaji wake kwa mfumo wa kupiga kura kwa njia ya kielektroniki akisisitiza hakutafanyika uchaguzi mwaka ujao kama ilivyopangwa ikiwa hakutafanyika mageuzi. 
 
Mfumo huo ulianzishwa mnamo 1996. Bolsonaro amesema uchunguzi dhidi yake uko nje ya mipaka ya katiba na ametishia kuchukua hatua nje ya katiba bila kufafanua.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...