Search This Blog

Tuesday, August 3, 2021

Babu wa Loliondo kuzikwa kesho Samunge


Mwili wa Mchungaji Ambikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo unatarajiwa kuzikwa kesho katika Kijiji cha Samunge, wilaya ya Ngorongoro mkoa wa Arusha sehemu ambayo alikuwa akitoa tiba ya mitidawa maarufu kama kikombe cha Babu.

Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mwangwala amethibitisha taarifa hiyo akiliambia Gazeti la Mwananchi, familia imekubaliana mazishi ya Mchungaji Ambikile kuwa Samunge.

Babu wa Loliondo alifariki Julai 30 akiwa na umri wa miaka 86, aliugua nimonia kali ambayo ilimsababisha kupata changamoto ya upumuaji na kupeleka kifo chake.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...