Search This Blog

Monday, August 9, 2021

Australia yaidhinisha matumizi ya chanjo ya Moderna

 Shirika la udhibiti wa madawa ya Australia na usimamizi wa bidhaa za tiba (TGA),limeidhinisha utumiaji wa chanjo mpya dhidi ya corona (Kovid-19) iliyotengenezwa na kampuni ya uzalishaji dawa ya Marekani ya Moderna kwa Waaustralia wenye umri wa miaka 18 na zaidi.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na TGA, matumizi ya chanjo ya Moderna, ambayo ilitajwa kuwa na ufanisi mkubwa dhidi ya Kovid-19 katika majaribio ya kliniki, iliidhinishwa.

Katika taarifa hiyo, ilibainika kuwa chanjo ya Moderna inaweza kutolewa kwa Waaustralia wenye umri wa miaka 18 na zaidi katika dozi 2 vya vipindi vya siku 28, na majaribio ya kliniki yanaendelea kwa matumizi ya chanjo hiyo kwa walio na umri wa kati ya miaka 12-17.

Chanjo iliyotengenezwa na Moderna imekuwa chanjo ya 4 ya Kovid-19 iliyoidhinishwa kutumiwa Australia baada ya chanjo zinazozalishwa na AstraZeneca, Pfizer-BioNTech na Johnson & Johnson.

Waziri Mkuu Scott Morrison, katika mkutano na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Canberra, alisema kuwa kwa idhini ya chanjo ya 4 ya Kovid-19 nchini, lengo la kutoa chanjo kwa asilimia 70 ya idadi ya watu litafikiwa ifikapo mwisho wa mwaka.

Akibainisha kwamba dozi milioni 1 za chanjo ya Moderna zitatolewa mwezi ujao na kwamba wamefanya makubaliano na Moderna kwa jumla ya dozi milioni 25 za chanjo, Morrison alisema kuwa wamechukua hatua muhimu katika mapambano dhidi ya Kovid-19.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...