Search This Blog

Wednesday, July 7, 2021

Waziri Simbachawene ashiriki mkutano wa Baraza la mawaziri wa asasi ya siasa, ulinzi na usalama jumuiya ya SADC kwa njia ya mtandao Dar


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akizungumza jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula, kabla ya kuanza kwa Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kwa njia ya Mtandao, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, leo Julai 7, 2021.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, akifuatilia Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kwa njia ya Mtandao, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, leo Julai 7, 2021.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akisalimiana na Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Meja Jenerali Jacob Mkunda, kabla ya kuanza Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kwa njia ya Mtandao, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, leo Julai 7, 2021.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Mawaziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Pamoja na Maafisa mbalimbali wakifuatilia  Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kwa njia ya Mtandao, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, leo Julai 7, 2021.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, akipitia nyaraka mbalimbali za Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kabla ya kuanza kwa Mkutano huo kwa njia ya Mtandao, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, leo Julai 7, 2021.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...