Search This Blog

Monday, July 12, 2021

Watu 11 wauawa na radi wakijipiga picha ‘selfies’ India


Radi imepiga na kuua takribani watu 11 na wengine kujeruhiwa huko Jaipur kaskazini mwa India siku ya Jumapili.

Watu hao walikuwa wakijipiga picha (selfie ) kwenye mvua wakiwa juu ya jengo eneo ambalo ni maarufu katika kivutio cha utalii.

Watu 27 walikuepo katika jengo hilona wakati kuta za ngome wakati tuko hilo likitokea – na baadhi waliripotiwa kuruka mpaka chini.

Radi huua watu wapatao 2,000 nchini India kwa wastani kila mwaka.

Afisa mkuu wa polisi aliviambia vyombo vya habari kuwa watu wengi waliouawa katika jengo hilo walikuwa vijana.

Jumapili peke yake, wameshuhudia zaidi ya vifo tisa vikiripotiwa katika jimbo la Rajasthan ambako Jaipur ipo , kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani.

Kiongozi wa jimbo hilo , Ashok Gehlot,alitangaza kutoadola 6700 sawa na 500,000 rupees kama fidia kwa familia zilizopoteza wapendwa wao.

Msimu wa mvua kubwa nchini India, hunyesha Juni mpaka Septemba.

Mamlaka ya hali ya hewa nchini India (IMD) imesema vifo vya radi vimeongezeka mara mbili nchini humo tangu miaka ya 1960 – sababu inayotajwa ni mabadiliko ya tabia nchi.

Takwimu zinasema matukio ya radi yanaongezeka kwa 30%-40% tangu mwanzoni na katikati ya mwaka -1990.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...