Search This Blog

Thursday, July 8, 2021

Wanajeshi wa Uingereza wajiondoa Afghanistan


Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson alisema kuwa idadi kubwa ya wanajeshi wa nchi yake walioko Afghanistan wamejiondoa na kwamba shughuli za kijeshi nchini Afghanistan zimekamilika.

"Tishio lililotuleta Afghanistan limepunguzwa sana." Kiongozi huyo alisema.

Katika hotuba yake kwenye Baraza la Wakuu, Johnson alitoa taarifa kuhusu kuondolewa kwa wanajeshi wa Uingereza wanaohudumu Afghanistan.

Johnson alieleza kuwa Afghanistan sio msingi tena wa al-Qaeda.

"Miaka ishirini baadaye, kambi za mafunzo zimepotea, uongozi wa al-Qaeda umesukumwa nje ya nchi. Hatupaswi kamwe kupoteza ukweli huu wa kimsingi." Boris alisema.

Johnson pia alifahamisha kuwa wanajeshi wengi wa Uingereza wameondoka nchini Afghanistan ingawa hakubaini tarehe kamili na kusema,

"Tishio lililotuleta Afghanistan limepunguzwa sana."

Akisisitiza kuwa vitisho vya kigaidi kutoka Afghanistan vinaendelea, Johnson pia alisema,

"akuna njia ya kijeshi ya ushindi kwa Taliban."

Akisisitiza kuwa uwepo wa kimataifa huko Afghanistan haukukusudiwa kuwa wa kudumu, Johnson alisema kuwa hakuna wakati mzuri wa kujiondoa.

Akisisitiza kwamba kuondoka kwa wanajeshi wa Uingereza kutoka Afghanistan haimaanishi kwamba nchi yake imeacha kuunga mkono Afghanistan, Johnson aliongezea kusema,

"Uingereza imeipa Afghanistan zaidi ya pauni milioni 100 za misaada ya maendeleo mwaka huu na kuchangia pauni milioni 58 kwa usalama wa kitaifa."

Waziri Mkuu Johnson alisema serikali ya Uingereza itaendelea kushughulikia suluhisho la mazungumzo huko Afghanistan na suluhisho hilo litahitaji kujumuisha Taliban.

Johnson alikataa wito wa wabunge wa uchunguzi juu ya uingiliaji wa Uingereza nchini Afghanistan na shughuli zitakazopatikana kwa hatua za baadaye.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...