Search This Blog

Thursday, July 8, 2021

Tahadhari ya shida ya uhamiaji barani Ulaya


Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban alisema kuwa hivi karibuni Ulaya itakabiliwa tena na shida ya uhamiaji.

Waziri Mkuu Viktor Orban, ambaye alifanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara ya Kigeni wa Hungary Peter Szijjarto huko Belgrade, mji mkuu wa Serbia, alikutana na Rais wa Serbia Aleksandar Vucic.

Akitoa taarifa katika mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari uliofanyika baada ya mazungumzo yao, Orban alisisitiza kwamba nchi za Ulaya ya Kati zinapaswa kuelewa kuwa masilahi yao ya mpito sio muhimu kuliko masilahi yao ya kudumu.

Orban alisema,

"Nchi zinahitaji kusaidiana. Kwa sababu mwelekeo wa upepo unaweza kubadilika, misaada wa nchi jirani inaweza kuhitajika. Ikiwa nchi za Ulaya ya Kati hazielewi hili, hakuwezi kuwa na mazungumzo ya utulivu."

Akikumbusha kuwa vita dhidi ya janga jipya la corona (Kovid-19) ambalo ni shida ya ulimwengu, bado vinaendelea kwa mafanikio, Orban pia alisema,

"Hivi karibuni tutakabiliwa na shida ya uhamiaji wa watu wengi, ambayo sote tunajua vizuri."



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...