Search This Blog

Monday, July 12, 2021

Ramaphosa: Hakuna sababu ya kufanya vurugu kupinga Zuma kufungwa


Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema hakuna sababu ya kufanya vurugu kupinga hatua ya kufungwa kwa rais wa zamani wa nchi hiyo, Jacob Zuma. 

Akizungumza jana, Ramaphosa amesema ghasia zinavuruga juhudi za kuujenga uchumi wa nchi hiyo wakati ambapo kuna janga la COVID-19. 

Amesema ingawa kuna walioumizwa na wenye hasira kwa sasa, hakuna uhalali wowote wa kufanya vurugu wala uharibifu wa mali. 

Ghasia zilizuka jana Jumapili kwenye miji kadhaa ya Afrika Kusini kupinga kifungo cha Zuma cha miezi 15 gerezani. 

Vurugu hizo zimeshuhudiwa zaidi kwenye jimbo la KwaZulu-Natal na kuenea hadi kwenye jimbo la Gauteng na jiji la Johannesburg. Waandamanaji walipora maduka na kuzuia barabara wakati wakiandamana kwenye miji hiyo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...