Rais wa Guatemala Alejandro Giammattei alisema kuwa hatua zitachukuliwa dhidi ya maandamano yanayomtaka ajiuzulu.
Barabara nyingi za mji mkuu nchini Guatemala, zilipambwa na mabango yanayodai kujiuzulu kwa Giammattei.
Giammattei, kwa upande mwingine, alionya kuwa maandamano yatapunguzwa na kusema,"Nadhani inatosha."
Giammattei pia alisema kuwa waandamanaji wanasababisha kuenea kwa aina mpya ya virusi vya corona (Kovid-19) kutokana na maandamano haramu ya kila wakati.
Kwa upande mwingine, Andrea Villagran, mmoja wa wabunge wa upinzani nchini, alisema kuwa haikubaliki kwa serikali kupunguza maandamano badala ya kudhibiti janga hilo.
Akifahamisha kuwa Giammattei anataka kukandamiza uhuru wa kujieleza, Villagran alisema, "Ikiwa kweli anataka kukabiliana dhidi ya janga hilo, kuna njia zingine ambazo hawatumii, kama vile kuhakikisha kuwa hatua zinafuatwa katika maduka makubwa, mikahawa, na maeneo ambapo watalii wako wengi zaidi."
Katika mji mkuu wa Guatemala, waandamanaji wapatao 300 walipinga usimamizi mbaya wa janga la Kovid-19 na kucheleweshwa kwa usafirishaji wa chanjo ya Sputnik dhidi ya Kovid-19 kutoka Urusi.
Waandamanaji hao walidai kujiuzulu kwa Giammattei kwa sababu ya kutoweza kuleta chanjo za kutosha za Kovid-19 nchini.

No comments:
Post a Comment