Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo amekanusha ripoti zinazosema kuwa ataunda chama chake cha kisiasa kabl aya uchaguzi mkuu unaotarajiw akufanyika nchini Nigeria mwaka 2023.
Mwishoni mwa juma, magazeti ya Nigeria yaliripoti kwamba rais huyu wa zamani atatekeleza mpango wake wa kuanzisha chama kipya cha kisiasa.
Katika taarifa, yake kwa vyombo vya habari Makamu wa rais Kehinde Akinyemi ameseam kuwa Obasanjo hana mipango ya kubuni chama kipya sasa au "katika siku za zijazo".
Obasanjo alisema wanaopiga propaganda wanapaswa kwenda kwenye hospitali ya magonjwa ya akili kwa ajili ya kufanyiwa kipimo cha skani.
"Nimemaliza suala la siasa lakini kwa nafasi yangu katika Nigeria na katika Afrika kwa ujumla, hupaswi kuzungumzia nafasi yangu duniani. Mlango wangu uko wazi wakati wote kwa wale wanaotaka kunsikiliza. Matendo yangu, nafasi yangu au ushauri wangu juu ya kitu fulani ambacho kinaendelea , ninaweza kufanya mambo yangu, bila kuungwa mkono na mtu yeyote au shirika lolote.
"Kama kungekuwa na chama ambacho Obasanjo angekiunda leo ambacho ni cha usalama, ukosefu wa ajira, njaa na umasikini, na changamoto nyingine zinazoikabiri nchi yangu, kingekuwa chama cha kuwaokoa watu wa Nigeria, kuunganisha nchi , kubuni amani na usalama na uthabiti pamoja na maendeleo , ”amesema Obasanjo.

No comments:
Post a Comment