Search This Blog

Tuesday, July 6, 2021

Mtoto wa rais wa zamani wa Mali asakwa na Interpol


Karim Keïta aliondoka Mali baada ya bababa yake kupinduliwaImage caption: Karim Keïta aliondoka Mali baada ya bababa yake kupinduliwa

Mmoja wa watoto wa kiume wa rais wa zamani wa Mali Ibrahim Keïta's, Karim, anasakwa na polisi ya kimataifaInterpol kuhusiana na kutoweka kwa mwandishi wa habari mwaka 2016.

Mwandishi wa habari wa Mali, Birama Touré, alipotea baada ya kukutana na Karim akimtaka atoe kauli yake katika katika taarifa aliyokuwa akiifuatilia ambayo ingemuharibia sifa.

Bw Karim alimshitaki muajiri wa mwandishi huyo, Le Sphinx, kwa kumuhusisha na kutoweka kwa mwandishi huo.

Mahakama nchini Mali ilipuuzilia mbali kesi hiyo lakini mhariri wa gazeti alikimbilia uhamishoni.

Bw Karim alikwepa kukamatwa na wanajeshi ambao walimpindua baba yake Agosti 2020.

Inasemekana anaishi katika nchi ya Ivory Coast.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...