Search This Blog

Wednesday, July 28, 2021

Msichana auawa kwa kuvaa jeans India


 

Taarifa za wasichana na wanawake wenye umri mdogo kushambuliwa kikatili na wanafamilia hivi karibuni zimekuwa zikigonga vichwa vya habari nchini India.

Matukio hayo pia yameangazia jinsi wasichana na wanawake wanakosa usalama hadi ndani ya nyumba wanazoishi na familia zao.

Wiki iliyopita, Neha Paswan, mwenye umri wa miaka 17, anadaiwa kupigwa hadi kufa na watu wa familia yake katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh kwasababu hawakupenda vile anavyovaa jeans.

Mama yake, Shakuntala Devi Paswan, aliiambia BBC Hindi kwamba msichana wake alikuwa amepigwa vibaya na fimbo na babu yake na wajomba zake baada ya kutokea kwa mabishano nyumbani juu ya nguo zake anazovaa katika kijiji cha Savreji Kharg wilayani Deoria, moja ya maeneo yenye maendeleo duni katika jimbo hilo.

"Alikuwa amefunga siku nzima kwendana na dini. Wakati wa jioni, akavaa suruali ya jeans na juu akawa na top au aina ya fulana kufanya ibada zake. Wakati babu na bibi yake walipinga mavazi yake, Neha alijibu kwamba jeans zilitengenezwa kwa ajili ya watu kuvaa", mama yake alisema.

Hoja hiyo ilizidi na kusababisha vurugu, anadai.

Shakuntala Devi alisema wakati binti yake akiwa amelala baada ya kupoteza fahamu, wakwe zake waliita gari wakisema wanampeleka hospitalini.

"Hawakuniruhusu niandamane nao kwa hivyo niliwatahadharisha jamaa zangu ambao walikwenda hospitali ya wilaya wakimtafuta lakini hawakumpata"



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...