Mke wa Rais Joe Biden wa Marekani, Dkt. Jill Biden (69) ameingia kwenye headlines baada ya kuonekana katika Jarida la Vogue, toleo la mwezi wa nane.
Kwenye toleo la hilo jipya, @drbiden amefunguka maisha halisi akiwa Ikulu na namna gani ameweza kuendelea kufundisha licha ya kuwa mke wa Rais pia na namna gani nchi ilivyobadilika tangu Rais Biden aingie madarakani.
Kuhusu @voguemagazine, hili ni jarida la kila mwezi la mitindo ya maisha la Marekani linaloangazia mada mbalimbali zikiwemo mitindo, uzuri na utamaduni na lilianza kama gazeti la kila wiki mwaka 1892, kabla ya kuwa jarida la kila mwezi miaka iliyofuata.
No comments:
Post a Comment