Search This Blog

Tuesday, July 13, 2021

Mke wa rais wa Ghana kurudisha marupurupu yake


Mke wa rais wa Ghana anataka kurejesha fedha za marupurupu anayopatiwa tangu rais aingie madarakani mwaka 2017, baada ya wananchi kulalamikia mshahara wake.

Vilevile Rebecca Akufo-Addo alisema hatakubali mshahara ambao ulipitishwa na bunge hivi karibuni.

Alisema katika taarifa yake kuwa aliamua kurudisha fedha zote ambazo alipewa kama ruzuku ambazo ni dola 151,618.

Alisema alikuwa hajaomba kulipwa na amepokea tu kutokana na wadhifa wake ingawa si rasmi.

Alisema ameamua kurudisha fedha hizo kutokana na maoni mabaya ambayo yametolewa na baadhi ya wananchi na kwa upande mwingine haipendezi , na kama inamuwasilisha kuwa fisadi, mbinafsi na mwanamke ambaye hajali maslahi ya raia wa Ghana”.

Mke wa rais na mke wa makamu wa rais wa GhanaImage caption: Mke wa rais na mke wa makamu wa rais wa Ghana

Wiki iliyopita,raia wa Ghana ameelezea kutokubaliana na maamuzi ya wabunge ya kuthibitisha mishahara ya wake wa rais na makamu wa rais kutokana na jukumu lao wanalopewa.

Wake hao walipangiwa kulipwa kiasi cha dola $3,500 (£2,500) kila mwezi , kiwango sawa na wanacholipwa mawaziri kufuatiwa mapendekezo yaliyotolewa na kamati ya bunge mwaka 2019.

Mke wa rais na mke wa makamu wa rais wamekuwa wanapokea marupurupu kwa miaka mingi kutokana na nyadhifa zao.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...