Search This Blog

Tuesday, July 13, 2021

Haruna Niyonzima kuagwa Yanga Julai 15


Uongozi wa klabu ya Yanga umewataka mashabiki wa klabu hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo wake dhidi ya Ihefu wa VPL utakauochezwa Julai 15 kwenye dimba la Mkapa ili kumuaga kiungo wake wa kimatifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima ambaye anamaliza mkataba wake msimu huu.

Yanga wameandika hayo kupitita ukurasa wake wa Instagram na kuipa heshima siku hiyo mahususi kwa kuiita 'Niyonzima Day'.

Ikumbukwe kuwa Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga mwaka 2011 akitokea klabu ya APR ya nchini Rwanda na kucheza kwa mafanikio makubwa hadi Julai mwaka 2017 ambapo alitimkia kwa watani wake wa jadi, Simba.

Niyonzima alikuwa kipenzi cha mashabiki wa Yanga kwa kuonesha uhodari wake wa kupiga pasi mpenyezo na madoido mengi akitokea eneo la kiungo mchezeshaji na hatimaye kuisaidia Yanga kubeba mataji yasiyopungua matatu ya Ligi kuu, moja la Shirikisho na kushiriki michuano ya Afrika.

Nyota huyo alianza misuguano ya kinidhamu na klabu yake ya Yanga hususani kuchelewa kurejea klabuni pindi aendapo nchini kwao Rwanda na baadae kutimkia Simba ambapo alifanikiwa kutwaa mataji mawili ya VPL na kuisaidia Simba kufika robo fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika.

Baada ya mkataba wake kumalizika kwa wekundu wa msimbazi Simba, Niyonzima akarejea Yanga mwezi Januari 2020 ambapo ameitumikia timu hiyo ya kwa mwaka mmoja na nusu, jumla ya miaka takribani saba ya mafanikio akiwa timu ya Wananchi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...