Waziri wa Ulinzi wa Afrika Kusini Nosiviwe Mapisa-Nqakula amesema wanajeshi wa Rwanda hawakutakiwa kuwasili Msumbiji kabla ya wale wa serikali za eneo hilo .
Waziri huyo alisema haikukubaliwa na wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) kwamba wanajeshi wa Rwanda wangefika kwanza.
"Inasikitisha kwamba kuja huko kunafanyika kabla ya kupelekwa kwa wanajeshi wa Sadc, kwa sababu kando na uhusiano wowote kati ya Rwanda na Msumbiji, mtu angetegemea Rwanda kwenda Msumbiji kwa muktadha wa agizo lililotolewa na wakuu wa nchi katika eneo la Sadc, " alisema.
Waziri huyo alisema hili lilikuwa suala la pande mbili, "hali ambayo hatuna udhibiti juu yake"
Wanajeshi wa Sadc wanatarajiwa kuwasili Msumbiji Alhamisi.
Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi alithibitisha kuwasili kwa wanajeshi wa Rwanda kusaidia vita dhidi ya wapiganani wa kundi la kigaidi ambalo limekuwa likifanya mashambulio katika wilaya za Kaskazini mwa nchi hiyo katika mkoa wa Cabo Delgado, tangu Oktoba 2017.

No comments:
Post a Comment