Search This Blog

Sunday, June 13, 2021

Zuchu apew Tuzo na Youtube

 


Mtandao wa YouTube umempa Tuzo (Gold Plaque) msanii Zuchu kwa kufikisha wafuatiliaji (subscribers) Milioni 1 (1,000,000) kwenye channel yake.

Tuzo hiyo imekuwa ikitolewa kwa watoa maudhui kwenye mtandao wa Youtube ambao channel zao zinafikisha wafuatiliaji (subscribers) kuanzia 100,000 na kuendelea.

Zuchu ambaye ana mwaka mmoja na miezi miwili tangu atambulishwe rasmi kujiunga na lebo ya WCB Wasafi, Aprili 8, 2020 anakuwa msanii wa kwanza wa kike nchini kufikisha Idadi hiyo kubwa ya wafuatiliaji (1M) kwenye mtandao huo.

Anayemfuata Zuchu YouTube kwa hapa nchini ni msanii Nandy ambaye anawafuatiliaji (781K), watatu ni Christina Shusho (327K), wanne ni Rose Muhando (300K) na watano ni Vanessa Mdee (281K).



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...