Hakuna ubishi katika majukwaa ya sanaa kwa sasa nchini, bila muziki wa ‘Singeli’ shoo haijakamilika. Licha ya hivyo mashabiki wanaona ni moja ya burudani muhimu kwao.
Sasa nyota wa muziki toka WCB Wasafi, msanii Zuchu leo Juni 15, ameachia wimbo wake wenye mahadhi ya Singeli. Wimbo huo unaitwa "Nyumba Ndogo". Tayari wimbo huo upo kwenye majukwaa yote ya kusikiliza muziki mtandaoni.
Hit maker huyo wa 'Sukari' @officialzuchu, huu unakuwa wimbo wake wa kwanza wenye mahadhi hayo na anaungana na wasanii wengine nchini kuachia wimbo wenye mahadhi ya Singeli, na hii ndio maana ya kupeleka singeli kimataifa.

No comments:
Post a Comment