Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Jumanne Juni 15, 2021 anatarajia kukutana na kuzungumza na vijana wa Kanda ya Ziwa kwa niaba ya vijana wa Tanzania katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
Tangu amekuwa kiongozi mkuu wa nchi, Samia amekutana na makundi mbalimbali na kupokea maoni yao, changamoto na namna ya kuzitatua na katika mkutano huo anatarajia kukutana na vijana zaidi ya 1,000.
Mamia ya vijana kutoka Mikoa ya Kanda hiyo tayari wamewasili uwanjani hapo kuanzia saa 12 asubuhi huku kukiwa na misururu ya vijana wengine nje ya uwanja wakisubiri kukaguliwa kwa ajili ya kuingia ndani.

No comments:
Post a Comment