Search This Blog

Saturday, June 19, 2021

Wawili wafa baada ya mgodi kuporomoka


 Watu wawili wamepoteza maisha na wengine wanne kujeruhiwa, baada ya duara moja katika mgodi wa dhahabu wa EMJ, uliopo Dutwa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, kuporomoka.


Kufuatia ajali hiyo serikali imetangaza kuufunga mgodi huo kwa muda wa siku tatu, ili kupisha ukaguzi wa wataalamu wa madini katika mduara mgodini hapo.


Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, akiwa na Kaimu Afisa Madini Mkazi wa mkoa wa Simiyu, Mhandisi Amini Msuya na maafisa wengine wa serikali, wamefika katika mgodi huo na kutangaza zuio hilo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...