Search This Blog

Sunday, June 6, 2021

Watu 2 wafariki kwenye shambulizi la bomu lililotokea Mogadishu nchini Somalia

Watu 2 waliuawa kwenye shambulizi la bomu lililotekelezwa katika eneo la soko huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.

Afisa wa Polisi wa Mogadishu Abdifatah Hassan alitangaza kuwa shambulizi la bomu lilitekelezwa katika soko dogo huko Ex-control Afgoye, lililoko mji mkuu wa Mogadishu.

Akibainisha kuwa watu 2 walipoteza maisha katika shambulizi hilo, Hassan alisema,

"Tunashuku mhusika wa shambulizi hilo alikuwa mshambuliaji aliyevaa vazi la kujitoa muhanga."

Hassan alifahamisha kuwa vikosi vya usalama vilitumwa katika eneo la tukio na uchunguzi ulianzishwa.

Kwa upande mwingine, katika taarifa za vyombo vya habari vya kitaifa, ilitangazwa kuwa watu 8 walijeruhiwa kwenye shambulizi hilo na walikuwa wakitibiwa.

Hakuna mtu yeyote ambaye amedai kuhusika na shambulizi hilo.

Shirika la kigaidi la Al-Shabab mara kwa mara huandaa mashambulizi yakilenga vikosi vya usalama na makaazi ya raia nchini Somalia.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...