Waziri wa Fedha wa Urusi Anton Siluanov alitangaza kuwa watamaliza kabisa hifadhi zao za dola katika Mfuko wa Kitaifa wa Ustawi, ambao una ujazo wa takriban dola bilioni 185 kwa mwezi.
Kulingana na mpango huo, kiwango cha euro, dhahabu na Yuan kitaongezeka badala ya kiwango cha dola.
Rais wa Urusi Vladimir Putin pia alitoa ujumbe kwamba wanalazimika kutekeleza mpango huu, ambao unafafanuliwa kama moja ya mikakati muhimu ya nchi hiyo.
Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi wa St.Petersburg, kiongozi wa Urusi alisema,
"Washirika wetu wa Marekani wanatulazimisha kufanya hivyo. Hatuachilii matumizi ya dola, tunalazimika kufanya hivyo."
Kulingana na Putin, wakati Marekanai ikitumia dola kama silaha ya vikwazo, inakata tawi lililo juu na inapunguza utegemezi kwa dola.
Akibainisha kuwa kampuni za nishati zinaweza pia kupunguza matumizi ya dola, Putin alisema,
"Hii itakuwa pigo kubwa kwa dola kama sarafu ya akiba duniani."
Kampuni za Nishati zinazodhibitiwa na serikali ya Urusi zimechukua hatua madhubuti kuongeza sehemu ya Yuan katika mafuta yanayosafirishwa kwenda China na euro katika mafuta na gesi kuuzwa kwa Ulaya.
Walakini, wataalam wanataja shida ambazo sekta binafsi nchini Urusi zitakabiliana nazo katika kuzoea mchakato huo kama kikwazo kikubwa katika mchakato wa kupunguzwa kwa uchumi wa Urusi.

No comments:
Post a Comment