Wanajeshi 7 wameripotiwa kupoteza maisha kwenye shambulizi lililotekelezwa dhidi ya vitengo vya kijeshi katika maeneo ya ndani ya nchi ya Mali.
Katika taarifa iliyotolewa juu ya tukio hilo, ilielezwa kuwa watu wenye silaha wasiojulikana walishambulia vitengo vya kijeshi katika mkoa wa Boni siku ya Ijumaa.
Ilisisitizwa kuwa wanajeshi 7 walipoteza maisha katika tukio hilo na washambuliaji waliweza kukabiliwa.

No comments:
Post a Comment