Ujerumani imetangaza kwamba itaondoa tahadhari yake ya kusafiri kwenda Uturuki kuanzia tarehe 1 Julai.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Heiko Maas, alitangaza kuwa tahadhari ya jamii ya kusafiri itaondolewa kuanzia tarehe 1 Julai hadi mikoa iliyo na kesi chini ya 200 za maambukizi ya corona (Covid-19) kwa wiki.
Hivyo basi, tahadhari na vizuizi vya usafiri dhidi ya Uturuki pia vitaondolewa.
Akionesha kuwa Covid-19 imebadilika, Maas alibainisha kuwa wataendelea kutoa tahadhari ya kusafiri kwa maeneo yenye hatari na maeneo yaliyokumbwa na aina mpya ya virusi.
Katika utekelezaji wa hatua za tahadhari huko Ujerumani, maonyo ya kusafiri hutolewa kwa mikoa yenye kesi zaidi ya 50 za maambukizi kwa watu elfu 100 kwa wiki.

No comments:
Post a Comment