Search This Blog

Saturday, June 12, 2021

Mgombea wa chama cha mrengo wa kushoto Pedro Castillo ashinda uchaguzi wa Urais Peru


Mgombea wa chama cha mrengo wa kushoto Pedro Castillo,  alishinda uchaguzi wa urais uliofanyika nchini Peru mnamo Juni 6.

Kulingana na data ya hivi karibuni iliyotolewa na Ofisi ya Michakato ya Uchaguzi wa Kitaifa (ONPE), katika duru ya pili ya uchaguzi, ambapo wagombea 2 waliopata kura nyingi katika raundi ya kwanza kwenye uchaguzi wa  Aprili 11, mgombea wa mrengo wa kushoto wa Chama cha Free Peru, Castillo, alipata ushindi kwa kupokea kura milioni 8,804,439 ambayo ni asilimia 50.19 katika uchaguzi.

Kulingana na matokeo yasiyokuwa rasmi huko Peru ambapo asilimia 100 ya kura zilihesabiwa, mgombea wa mrengo wa kulia wa chama cha Power Keiko Fujimori alifuatia katika nafasi ya pili kwa kura milioni 8,735,472 ambayo ni asilimia 49.80.

Wakati bado haijulikani ni lini matokeo rasmi yatatangazwa nchini licha ya kukamilishwa kwa shughuli ya kuhesabu kura, wafuasi wa Castillo walianza sherehe na kutangaza ushindi.

Kwa upande mwingine, Fujimori alitangaza kwamba watapinga takriban kura elfu 200 katika masanduku 86 ya kura, wakisema kwamba kulikuwa na udanganyifu katika uchaguzi.

Katika taarifa iliyotolewa wakati wa mchana, Castillo alisisitiza kwamba watasubiri matokeo rasmi yatangazwe kwa utulivu na amani, na kuwataka wafuasi wake kutosababisha uchochezi.

Mgombea atakayeshinda uchaguzi atachukua madaraka ya serikali mpya Julai 28, ambayo ni siku ya kumbukumbu ya miaka 200 ya uhuru wa Peru, na atahudumu kwa muhula wa 2021-2026.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...