Serikali ya Malaysia ilijibu hatua ya ukiukaji wa anga ya Malaysia uliotekelezwa hapo jana na ndege 16 za kivita za China.
Katika taarifa iliyoandikwa, Waziri wa Mambo ya Nje Hishamuddin Hussein alisema kuwa Malaysia itatuma barua ya kidiplomasia kupinga ukiukaji wa anga wa serikali ya China, kulingana na maelezo ya Kikosi cha Anga cha Malaysia hapo jana.
Hishamuddin alisema,
"Balozi wa China nchini Malaysia ataitwa kwa Wizara hiyo kutoa maelezo kuhusu ukiukaji wa anga na mamlaka ya Malaysia na ndege 16 za kivita."
Akibainisha kuwa atawasilisha hofu ya Malaysia kuhusu ukiukaji wa anga kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi, Hishamuddin pia alisema,
"Utayari wa Malaysia kuanzisha uhusiano wa kirafiki na kila nchi haimaanishi kwamba itahatarisha usalama wake wa kitaifa. Malaysia itabaki na azimio la kuhifadhi enzi na heshima yake."
Katika taarifa iliyoandikwa kutoka Ubalozi wa China nchini Malaysia, ilielezwa kuwa ndege hizo zilikuwa za mazoezi ya kawaida ambazo hazikulenga anga ya Malaysia.
Katika taarifa ya maandishi iliyotolewa hapo jana na Kikosi cha Anga cha Malaysia, iliripotiwa kuwa mnamo Mei 31, ndege 16 za Kikosi cha Anga cha China zilionekana kukiuka anga ya Malaysia.

No comments:
Post a Comment