Search This Blog

Wednesday, June 2, 2021

Maiga achaguliwa kuwa Waziri Mkuu Mali


Assimi Goita, ambaye alikuwa nyuma ya mapinduzi ya kijeshi nchini Mali na kujitangaza mwenyewe kuwa rais, alimteua Choguel Maiga kuwa Waziri Mkuu wa nchi.

Shirika rasmi la habari la Mali Amap, lilitangaza kuwa Choguel Maiga, ambaye ni mhusika wa sehemu ya jukwaa la upinzani la M5-RFP, aliteuliwa kama Waziri Mkuu na Goita.

Maiga mwenye umri wa miaka 63 ambaye pia ni Mwanzilishi wa Harakati ya Uzalendo, aliwahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara kutoka mwaka 2002 hadi 2007, na Waziri wa Uchumi wa Dijitali na Mawasiliano kutoka mwaka 2015 hadi 2016.

Maiga alikuwa miongoni mwa watu mashuhuri wa jukwaa la upinzani la M5-RFP, ambalo lilichukua hatua kufuatia kujiuzulu kwa Rais Ibrahim Boubacar Keita, ambaye alipinduliwa na mapinduzi ya kijeshi mnamo Agosti 18, 2020.

Kanali Goita, ambaye pia alikuwa nyuma ya mapinduzi ya mwaka jana na aliwahi kuwa Makamu wa Rais wakati wa mchakato wa mpito, aliamuru kuzuiliwa kwa maafisa wengi wa ngazi za juu, akiwemo Rais Bah Ndaw pamoja na Waziri Mkuu Moctar Ouane, kwa madai kwamba baraza la mawaziri lililobadilisha Mei 24 halikuambatana na taratibu zilizokuwa zimetolewa.

Goita baadaye alijitangaza kuwa Rais wa nchi ya Mali.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...