Search This Blog

Monday, June 21, 2021

Mawe ya yaliyokimbiliwa Afrika Kusini yagundulika kuwa hayakuwa Almasi


Wataalam wa machimbo ya migodi wamebaini kuwa mawe yaliyopatikana KwaHlati katika Ladysmith, KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini ni vipande vya madini ya quartz na, sio Almasi.

Jopo la wataalamu lilitoa tangazo Jumapili.

Zaidi ya watu 1,000 walikimbilia katika kijiji cha KwaHlatikusaka kuyasaka mawe hayo ambayo waliamini yalikuwa ni Almasi.

Watu walisafiri kutoka maeneo mbali mbali kote nchini Afrika Kusini kujiunga na wanavijiji ambao walikuwa wakiyachimba tangu Jumamosi , baada ya kusikia kuwa vipande hivyo vya mawe vilikuwa ni Almasi ambayo ingewatajirisha.

Uvumbuzi wa mawe haya utabadilisha maisha, alisema mchimbaji mmoja Mendo Sabelo aliyekuwa amebeba vipande vya mawe hayo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...