Search This Blog

Tuesday, June 8, 2021

Maji kukosekana June 8 hadi 9, DAWASA waomba radhi


Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar-es-salaam (DAWASA) inawataarifu wananchi na wakazi wa Bagamoyo hadi Kigamboni kuwa huduma ya majisafi itakosekana kwa saa 24 kuanzia tarehe 8/6/2021 asubuhi hadi 9/6/2021.

Sababu ya kukosekana kwa maji ni matengenezo ya bomba kuu la usambazaji maji 54 linalotokea katika matenki ya chuo kikuu Ardhi eneo la Victoria na Makumbusho baada ya kupasuka.

Maeneo yatakayoathirika ni Mji wa Bagamoyo, Vijiji vya Zinga, Kerege, Mapinga, Bunju, Boko, Mivumoni, Kawe, Kinondoni, Ilala, Temeke, Uwanja wa ndege, Tegeta, kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi beach, Mlalakuwa,Mwenge, Mikocheni, Msasani, sinza, kijitonyama, oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, katikati ya jiji (City center), Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati, hospitali ya Rufaa Mhimbili, Kigamboni Navy na Ferry

DAWASA inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...