Search This Blog

Wednesday, June 9, 2021

Mahakama ya UN yathibitisha kifungo cha maisha kwa Ratko Mladic

Karibu miaka 26 baada ya mauaji ya halaiki ya Srebrenica, Mahakama Maalum ya Uhalifu wa Kivita ya Umoja wa Mataifa imethibitisha adhabu ya kifungo cha maisha jela iliyotolewa kwa aliyekuwa jenerali wa jeshi la Waserbia wa Bosnia Ratko Mladic kwa mauaji ya karibu wanaume na wavulana 8,000 katika eneo la Srebrenica na uhalifu mwingine ikiwemo mzingiro wa Sarajevo ambapo maelfu ya watu waliuawa. 

Uamuzi huo wa mahakama una maana kuwa Mladic amepoteza rufaa yake ya mwisho dhidi ya hukumu yake kwa mauaji ya kimbari. Mladic, mwenye umri wa miaka 78, ambaye baadae alifahamika kama "Mchinjaji wa Bosnia" wakati wa Vita vya Bosnia vya mwaka wa 1992 hadi 95, alitaka afutiwe mashitaka. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewashukuru majaji na wale waliohusika katika kesi hiyo kutokana na bidii yao kwa miongo mingi. Muendesha mkuu wa mashitaka wa mahakama hiyo Serge Brammertz aliukaribisha uamuzi huo na kuwaambia wafuasi wa Mladic kuwa ni wakati wa kukubali ukweli.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...