Search This Blog

Wednesday, June 9, 2021

Kenya kufunga maelfu ya nambari ya siri ya walipa kodi wasiowajibika


Mamlaka ya mapato nchini Kenya (KRA) inatarajiwa kuzifungia jumla ya nambari za siri 66,269 za kulipa kodi ambazo hazitumiki kufikia Alhamisi wiki hii, ripoti za vyombo vya habari nchi humo zinasema .

Wamiliki wa nambari hizo za siri za kulipa kodi ambao ni pamoja na watu binafsi na mashirika ya biashara huenda wakafutiwa usajili malipo ya ushuru wa bidhaa.

Walipa kodi watakaoathiriwa watazuiwa kutoza ada ya ushuru wa bidhaa katika biashara zao na huenda wakakabiliwa na vikwazo vingine vya utozaji ushuru.

Hatua kama hiyo pia itachukuliwa dhidi ya watu ambao hawajakuwa wakijaza fomu ya kuthibitisha wanalipa kodi kwa mujibu wa sheria.

“Kufutiwa kwa jukumu la kulipa ushuru wa bidhaa ni mpango unaoendelea, utawaathiri walipa kodi ambao hawatajaza fomu ya kila mwezi ya kuthibitisha wamelipa ushuru wa bidhaa au wale ambao hawaoneshi jinsi walivyolipa ushuru huo kila mwezi miongoni mwa mambo mengine,” KRA ilisema katika taarifa yake kwa umma.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...