Kiongozi maarufu wa kikundi cha wapiganaji wa Kipalestina Hamas, Yahya Sinwar, amekuwa na nyadhifa za ngazi ya juu za jeshi na siasa katika vugu vugu la Hamas, na sasa ni kiongozi wa makao makuu ya kundi hilo mjini Gaza.
Yahya Sinwar, alizaliwa mwaka 1962 katika kambi ya wakimbizi ya Khan Yonis iliyopo Gaza.
Alikamatwa na kuhukumiwa kifungo cha jela cha miaka minne mwaka 1988, bada ya kupatikana na hatia ya kuunda kikundi cha al-Jihad w cha Da'wah, kikosi cha usalama wa ndani cha Hamas .
Wakati alipoanzisha tawi hili kulikuwa na harakati za kwanza dhidi ya Israeli.
Aliachiliwa kutoka gerezani mwaka 2011 wakati Israeli ilipokubali kutoa wafungwa wa Kipalestina gerezani ili ipewe mwanajeshi wake,Gilad Shalit.
Miaka miwili baada ya kuachiliwa kwake, alichaguliwa kuwa mkuu wa ofisi ya Hamas.
Mwaka 2015 Marekani iliongeza jina lake kwenye orodha ya magaidi wa kimataifa.
Mnamo mwaka 2017, alichaguliwa kama mkuu wa kikundi cha Hamas katika Gaza.
Kaka yake mdogo, Mohammed Sinwar, anayefahamika zaidi kwa jina la Abu-Ibrhaim, alikuwa kamanda wa Kikosi cha Hamas kinachoitwa Al-Qasam Brigade.

No comments:
Post a Comment