Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken, aliwasiliana na mawaziri wa mambo ya nje kutoka Misri, Saudi Arabia, Qatar, Pakistan na Ufaransa na kujadili juhudi za kumaliza ghasia na kuhakikisha amani katika mzozo wa Israel na Palestina.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Ned Price alitoa taarifa kwa maandishi kuhusu mawasiliano ya simu ya Blinken na mawaziri wenzake kutoka nchi 5.
Wakati yake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Semih Shukri, Blinken alitoa wito kwa pande zote za Israel na Palestina kupunguza mvutano na kumaliza vurugu, na akaishukuru Misri kwa juhudi zake katika suala hili.
Katika mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia Faisal bin Farhan Al Saud, Blinken alizungumzia juhudi za kukomesha vurugu huko Israel, Gaza na Ukingo wa Magharibi, na kuelezea kuwa Wapalestina na Waisrael wanateseka kutokana na kupoteza maisha.
Akifahamisha kuwa Wapalestina na Waisrael wana haki sawa ya kuishi kwa uhuru, uaminifu, utu na ustawi, Blinken na Al Saud pia walizungumzia hali ya hivi karibuni nchini Yemen na maendeleo ya sasa kuhusu haki za kibinadamu huko Saudi Arabia.
Blinken pia alizungumzia michakato ya kumaliza ghasia zinazoongezeka katika mzozo wa Israel na Palestina katika mkutano wake na mwenzake wa Qatar, Mohammed bin Abdurrahman Al-Thani, na mwenzake wa Ufaransa, Jean-Yves Le Drian.
Blinken pia aliwasiliana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan Mahmud Qurayshi ambapo alisisitiza umuhimu wa kuendeleza msaada wa Pakistan kwa mchakato wa amani wa Afghanistan na kutoa ujumbe kwamba ushirikiano kati ya Marekani na Pakistan utaendelea.

No comments:
Post a Comment