Aina mpya ya virusi vya corona ambavyo vinaweza kusambazwa kutoka kwa mbwa kwenda kwa mwanadamu na kusababisha homa ya mapafu vimegundulika nchini Malaysia.
Kulingana na utafiti uliochapishwa katika jarida la Magonjwa ya Kuambukiza ya Kliniki lenye makao makuu yake Marekani (USA), sampuli za kamasi za pua zilizochukuliwa kutoka kwa wagonjwa 305 wa homa ya mapafu waliolazwa hospitalini huko Sarawak, Malaysia mnamo 2017-2018 zilichunguzwa.
Ilibainika kuwa wagonjwa 8 ambao sampuli zao zilichunguzwa, haswa chini ya umri wa miaka 5, walipata aina mpya ya virusi vya corona vinavyoonekana kwa mbwa.
Wanasayansi, ambao walitaja aina mpya ya virusi vya corona kuwa "CCoV-HuPn-2018", walisema kwamba virusi hivi vina sifa sawa na virusi vilivyoonekana hapo awali kwa paka na nguruwe.
Ilisisitizwa kwa utafiti zaidi unaendelea kuthibitisha ikiwa virusi vinaambukizwa kutoka kwa mwanadamu mmoja kwenda kwa mwingine.
Imetangazwa kwamba ikiwa vitabainishwa kuambukizwa kati ya wanadamu, virusi hivi vitakuwa ni vya 8 vilivyogunduliwa hadi sasa na husababisha magonjwa kwa wanadamu.

No comments:
Post a Comment