Search This Blog

Sunday, May 23, 2021

Muungano wa Wanahabari wa Palestina wawataka maafisa wa mitandao ya kijamii kuchunguzwa juu ya Israel


Muungano wa Wanahabari wa Palestina umewataka maafisa wa mitandao ya kijamii kujumuishwa katika uchunguzi juu ya Israel.

Kufuatia mashambulizi ya Israel katika maeneo ya Wapalestina, tagi za mitandao ya kijamii zilianzishwa kwa mshikamano na Wapalestina, lakini nyingi zilipigwa marufuku kwa madai ya "kukiuka kanuni."

Tabia hii ya matumizi ya mitandao ya kijamii maarufu kama vile Facebook, Twitter na Instagram ilikosolewa sana.

Muungano wa Wanahabari wa Palestina pia unaamini kuwa tovuti za mitandao ya kijamii zinahusika katika uhalifu dhidi ya Palestina na maamuzi ya kuzuia.

Muungano huo uliwataka maafisa kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kujumuishwa katika uchunguzi wa kimataifa juu ya mapigano ya Israel na uhalifu dhidi ya ubinadamu.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...