Search This Blog

Sunday, May 30, 2021

Viongozi wa ECOWAS wajadili mzozo wa Mali

 


Viongozi wa nchi za Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi (ECOWAS), wanakutana leo Jumapili nchini Ghana kujadili mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Mali. 

Viongozi hao wataamua kuhusu hatua ya kuchukua kufuatia mapinduzi ya pili katika kipindi cha miezi 9. Kiongozi wa kijeshi wa Mali Kanali Assimi Goita alialikwa kuhudhuria kikao cha mashauriano hapo jana kabla ya kuanza kwa mkutano wa leo wa kilele. 

Duru za jeshi na maafisa wa uwanja wa ndege zimesema Goita aliwasili mjini Accra jana Jumamosi akitokea Bamako. 

Goita alihudumu kama makamu wa rais tangu alipoongoza mapinduzi mwezi Agosti mwaka uliopita yaliyomuondoa madarakani rais aliyechaguliwa kidemokrasia Ibrahim Boubacar Keita. 

Nafasi ya rais na waziri mkuu zimekuwa zikishikiliwa na viongozi wa kiraia, Bah Ndaw na Moctar Ouane kufuatia shinikizo kutoka kwa jumuiya ya ECOWAS ambayo imekuwa mpatanishi.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...