Search This Blog

Friday, May 28, 2021

Vikosi vya kigeni kuisaidia Msumbiji dhidi ya Magaidi


Viongozi wa baadhi ya mataifa ya kusini mwa Afrika wamekubali kuanzisha jeshi la pamoja la dharura ambalo litakabiliana na wanamgambo wa kiislamu katika mkoa wa kaskazini wa Cabo Delgado nchini Msumbiji.

Viongozi wa SADCwamekubaliana katika mkutanosiku ya Alhamisi kwamba jeshi hilo litaongozwa na Msumbiji.

Litashirikisha wanajeshi kutoka mataifa ya SADCijapokuwa hakuna idadi ya wanajeshi iliotajwa.

Kuna hofu kwamba mashambulizi ya Msumbiji huenda yakatapakaa jadi mataifa Jirani.

Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi, ambaye pia ndiye kaimu mwenyekiti wa SADC amesema kuwa hatua hiyo itasaidia katika kuwapunguza nguvu wanamgambo hao mbali na kuharibu vyanzo vyao vya silaha na mikakati.

Alitetea ushirikiano huo aliodai kwamba unaweza kwa urahisi kukabiliana na ugaidikaskazini mwa Msumbiji bila kukatiza tamaa za mataifa mengine yanayotoa usaidizi, ndugu na mashirika ya kimataifa.

Marekani Ufaransa na Ureno iliotawala eneo hilo tayari zilikuwa zimeonesha hamu ya kutaka kutoa usaidizi wa kiufundi na mafunzo kwa wanajeshi wa Msumbiji.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...