Baraza la Mawaziri nchini Ujerumani, liliamua kupunguza vizuizi na hatua za corona (Covid-19) kwa watu ambao walipewa dozi ya pili ya chanjo.
Waziri wa Sheria Christine Lambrecht alisema kwenye taarifa aliyoitoa katika mji mkuu wa Berlin kwamba kanuni iliyoandaliwa kwa ajili ya kupunguza hatua za Covid-19 kwa wale ambao walikuwa wamepewa chanjo kamili ilikubaliwa katika Baraza la Mawaziri.
Kulingana na kanuni iliyopitishwa na Baraza la Mawaziri, wale ambao wamepewa chanjo kamili na wale waliopata Covid-19 na kupona watashughulikiwa kwa kiwango sawa na wale waliopata matokeo hasi ya vipimo.
Kwa hivyo, wale ambao wamepewa chanjo kamili na kupona watapunguziwa vizuizi na kuruhusiwa kutoka nje, ingawa jukumu la kuvaa barakoa na kuzingatia sheria ya masafa kati ya watu zitaendelea.
Kanuni hiyo inatarajiwa kujadiliwa katika Bundestag na Baraza la Wawakilishi la Jimbo la Shirikisho (Bundesrat) baadaye wiki hii na kuanza kutumika mwishoni mwa wiki.
Katika kampeni inayoendelea ya chanjo nchini Ujerumani, kufikia Mei 3, dozi ya kwanza ya chanjo ya Covid-19 ilipewa watu 23,852,426 na dozi ya pili kwa watu 6,771,476
Hivyo basi, dozi 30,623,902 za chanjo zimeweza kutolewa nchini tangu Desemba 27, 2020.

No comments:
Post a Comment