Search This Blog

Monday, May 10, 2021

TAKUKURU Masasi yawafikisha Viongozi wawili wa AMCOS Mahakamani

 


Na Hamisi Nasri, Masasi.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa( TAKUKURU) wilayani Masasi mkoani Mtwara imewafikisha Mahakamani katika mahakama ya wilaya ya Masasi viongozi wawili wa Chama Cha Msingi Mkululu  (AMCOS)   wakikabiliwa na kesi ya  uhujumu uchumi.

Viongozi hao ambao wamefikishwa katika mahakama hiyo ni Rashidi Hamisi ambaye ni mwenyekiti wa Chama hicho cha Msingi na katibu wake, Omari Timamu.

Kesi hiyo namba 8 ya mwaka 2021 imesomwa mwishoni mwa wiki katika mahakama hiyo mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo ya wilaya ya Masasi, Bastita Kashusha.

 Akisoma kesi hiyo mbele ya mahakama hiyo, mwendesha mashtaka wa Takukuru wilaya ya Masasi, Charles Mtungila alidai mahakamani hapo kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.

Alidai kuwa kosa la kwanza ni kutumia nyaraka za uongo kwa lengo la kumdanganya  mwaajili.

Mwendesha huyo wa mashtaka wa Takukuru alidai kuwa kosa la pili ni kujipatia fedha shilingi milioni tatu kwa udaganyanyifu.

Watuhumiwa hao wawili walikana mashtaka yao na kwamba mahakama iliwataka washtakiwa hao kuweka bondi ya maneno ya shilingi milioni tatu kila mmoja ili kuweza kupata 

Kesi hiyo imeaharishwa hadi tarehe 21 Mei mwaka 2021 itakapo somwa tena 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...