Raia 7 wameuawa katika shambulizi la Taliban katika mkoa wa Kapisa nchini Afghanistan.
Msemaji wa Idara ya Polisi ya Kapisa Shayık Shurish amesema kuwa wanamgambo wa Taliban walishambulia harusi katika kijiji cha Enarcuy.
Akiripoti kuwa raia 7 wamepoteza maisha na raia 4 wamejeruhiwa katika shambulizi hilo, Shurish amesema kuwa watoto walikuwa miongoni mwa waliopoteza maisha.
Taliban kwa upande wao wamedai kuwa shambulizi hilo la lilitekelezwa na vikosi vya usalama.
Kwa upande mmoja, juhudi za kuhakikisha utulivu nchini zikiwa zinaendelea, mashambulizi nayo yamepamba moto.
Mbali na hapo, kulingana na serikali ya Afghanistan ghasia zimeongezeka nchini tangu majeshi ya kigeni yalipoanza kujiondoa kwa takriban mwezi mmoja.
Wawakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan (UNAMA) wametangaza kuwa raia 573 waliuawa nchini Afghanistan katika robo ya kwanza ya mwaka 2021.

No comments:
Post a Comment