Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema taifa lake litakuwa la kwanza kuleta chanjo ya mRNA barani Afrika wakati bara hilo likipambana na janga la virusi vya corona.
“Rwanda inafanya kazi na washirika ili kuwa ya kwanza kutengeneza chanjo ya mRNA barani Afrika,” Kagame amesema katika mkutano wa kwenye mtandao wiki hii katika mkutano ulioitishwa na jopo huru la kukabiliana na janga la corona ingawa hakutoa ufafanuzi.
Waziri wa afya wa Rwanda, Luteni Kanali Dkt.Tharcisse Mpunga ameliambia shirika la utangazaji la Rwanda kuwa mjadala huo ulikuwa ni wa kuleta kiwanda cha chanjo Rwanda.
“Hii inaweza kuwa hatua kubwa kwa Rwanda na Afrika kupata chanjo …tunategemea kuwa punde mijadala hii itazaa matunda”, Dkt Mpunga salisema Alhamisi usiku.
“Ikiwa kama Afrika bado inategemea chanjo kutoka mabara mengine , tutakuwa nyuma kwenye foleni mara zote panapokuwa na uhaba”, Bwana Kagame alisema hayo kwenye mjadala ulioongozwa na aliyekuwa rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf na waziri mkuu wa zamani wa New Zealand Helen Clark siku ya Jumanne.
Mamlaka ya Rwanda haijatoa ufafanuzi ya namna kiwanda hicho kitawekwa Rwanda.
Makampuni ya dawa ya Marekani na Ujerumani - Pfizer Inc. na BioNTech SE - walishirikiana kutengeneza chanjo ya mRNA vkukabiliana na Covid-19, kama Moderna Inc.
Afrika ina viwanda vichache vya uzalishaji wa aina yeyote ya chanjo na vile vilivyopo vingi huwa vinaweka vifungashio na kusambaza - ila sio kutengeneza wenyewe.
Chanjo ya mRNA inatofautiana na usambazaji wake na kuwa mshirika wa utengenezaji na RNA, au kemikali inayofahamika kama ribonucleic, kulinda mwili dhidi ya vimelea vya magonjwa. Pfizer Inc., pamoja na BioNTech SE, ilianzishwa na chanjo ya mRNA kupambana na Covid-19, wakati Moderna Inc.ilithibitishwa kuwa bora zaidi ya zile zilizotengenezwa na makampuni mengine yanayotumia namna nyingine ya utengenezaji.
“Nilikuwa na fursa ya kufanya mawasiliano na makampuni kadhaa ya chanjo haswa nikilenga mjumbe wa teknolojia ya RNA iliyotumika kwenye Moderna na Pfizer,” Kagame alisema mwezi uliopita.
“Tumekuwa tukishiriki katika mijadala na baadhi ya viongozi wengine barani kwetu lakini tunataka kujadilina zaidi kuhusu hili na wengine.”
Mwezi Februari, Rwanda ilianza kutoa chanjo kwa wahudumu ambao wako kwenye hatari ya maambukizi wakati taifa hilo likiwa na idadi ndogo ya chanjo, baadhi wakiwa wamepata chanjo ya Pfizer-BioNTech.
Zaidi ya watu 350,000 wamepata chanjo ya corona nchini humo, wizara ya afya imesema.
Zaidi ya dozi milioni 17 za chanjo ya corona zimepelekwa Afrika ambayo ina watu bilioni 1.3 ambapo kiwango kilichotolewa ni chini ya 2% ya dozi milioni 780 zilizotolewa duniani , WHO imesema.

No comments:
Post a Comment